• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Monday, August 6, 2012

    AFRICA POLITICAL NEWS: RAIS WA MAURITANIA ASEMA UPINZANI NCHINI HUMO NI DHAIFU



    Rais wa Mauritania amelitaja ombi la wapinzani waliomtaka ajiuzulu uongozi kuwa ni ishara ya udhaifu wao. 
    Rais Muhammad Ould Abdulaziz wa Mauritania amesema leo kuwa lengo la wapinzani wanaomtaka aondoke madarakani ni kufunika kushindwa kwao kujipatia kura za wananchi. Rais wa Mauritania ameongeza kuwa viongozi wa upinzani wote walishiriki kwenye mchuano wa uchaguzi wa rais lakini walishindwa kupata kura za wananchi wa Mautritania. Rais Muhammad Ould Abdulaziz amesema anataraji kuwashinda tena wapinzani wake katika kila uchaguzi utakofanyika nchini humo. Rais Abdulaziz amesisitiza pia kufungamana nchi yake na suala la kuwa na uhusiano mwema na majirani zake na kueleza kuwa Mauritania haina tatizo lolote na majirani zake.

    No comments:

    3500K