• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Thursday, August 23, 2012

    STORI KAMILI KUHUSU HII FAMILIA YA KANUMBA SHINYANGA KUREKODI MOVIE MWEZI UJAO HAPA NYUMBANI KWAO.


    Kaka pamoja na wadogo zake Kanumba kwa upande wa baba, Mjanaheri ni huyo wa kwanza kulia.
    Imefahamika kwamba baadhi ya wanafamilia wa Marehemu Steven Kanumba mkoani Shinyanga wameshakamilisha mipango ya kucheza movie yao ya kwanza toka watangaze kuanza kuigiza.
    Kambini wanaingia tarehe 30 August 2012, movie wanaanza kucheza tarehe 3 septemba inaitwa Nasikia kuitwa ambapo watakaocheza ni mdogo wake Kanumba kwa upande wa baba aitwae Mjanaheri pamoja na baba mzazi ambapo itachezwa hukohuko Shinyanga.

    Movie imetungwa na Mwalimu Emanuel Yahewa ambae ni ndio msimamizi wa kikundi cha Taisee art kilichopo chini ya kanisa la AICT Kambarage  ambapo Marehemu ndipo alikua anaimbia kwaya, alijifunzia gitaa na uigizaji hapo hapo.
    Nyumbani kwa kina Kanumba Shinyanga.
    Mwanzilishi wa kikundi hicho chenye watu 39 ni Mjanaheri Kanumba ambae amesema movie itakua imekamilika ndani ya mwezi mmoja, kampuni inayoitengeneza ni RJ ya Ray Vicent Kigosi lakini director ni Magulu ambae alikua Director wa Kanumba kwa miaka saba lakini kampuni ya Kanumba haitohusika hata kidogo na utengenezaji wa movie hiyo, baba mzazi wa Marehemu Kanumba atashiriki kucheza pia kama kiongozi wa sungusungu.
    Stori yake haihusiani sana na maisha ya Kanumba japo mwishoni mwa hiyo movie kuna baadhi ya vitu vyake vitahusishwa, zikiwemo nyimbo na sehemu kidogo ya maisha yake.
    Millard Ayo na baba mzazi wa Kanumba nyumbani kwao Shinyanga.
    Mwezi mmoja baada ya kifo cha Kanumba nilipata nafasi ya kufanya interview na familia yake Shinyanga, wadogo zake wanne walinihakikishia kwamba wako tayari kuingia kwenye soko la movie Tanzania kwa sababu uwezo wanao na wanataka kuliendeleza jina la ukoo wao.
    Hili ndio Kanisa Marehemu Kanumba alipojifunzia uigizaji na kuimba kwaya, na ndio kanisa ambalo linasimamia hiki kikundi cha uigizaji anachokiongoza mdogo wake. 
                             chanzo ni millardayo

    No comments:

    3500K