Siku
ya 17 ya mwezi wa 6 mwaka 2012 itakuwa ni masoniq day kulingana na
calendar zinavyoonyesha, siku ambayo ina historia kubwa na nyingi
kidunia mbali na historia mpya itakayotengenezwa kwenye usiku wa
kuzindua video mpya ya Christopher kweka, notorious wa bongo, mjukuu wa
lucifa, p.g kweka known us Baghdad itwayo tom boy. Licha ya kuzindua
album masoniq day ndio siku ambayo itatatua utata ama vuguvugu
lililokuwa likiendelea chini kwa chini kuhusiana na maelewano mabaya
baina ya mtoto wa ilala kiongozi wa kundi la lafamilia chid benz, na mtu
mzima Baghdad kwa tetesi eti huwa wanatambianaga mara kwa maraa
wanapokutana back stage. Kwa mara ya kwanza chidi benzi alikutana na
Baghdad Azania sec school shule ambayo alikuwa anasoma Baghdad kwa
kipindi hicho na chidi kukalishwa kwenye stage mpaka kupelekea benzino
kurudia nyimbo yake pendwa cha ngoma itambae akitegemea ingeweza
kubadilisha matokeo lakini haikuwa kama mawazo yake ingawa ma fun wake
waliamini ni kwa sababu Baghdad alikuwa nyumbani kwao! Kwa mara ya pili
mfalme wa ilala alichukua point zake 3 mapema wakiwa ugenini wote
wawili, ilikuwa ni kwenye tamasha la sauti za busara linalofanyikaga
mara moja kwa mwaka visiwa vya Zanzibar nchini Tanzania, takwim
zinaonyesha kuwa chidi alimpa ofa Baghdad ya kuwa kwenye ile mechi
akitoa dro ushindi wake. huku Baghdad akijitahidi kutaafuta hata droo
ili ajitete ila matokeo yalikuwaa ni tatu bila! Sasa imepita zaidi ya
miaka 3 tangu wakutane sauti za busara na kutarajiwa kukutana tena pande
za maisha club kwenye siku ya uzinduzi wa video mpya ya Baghdad iitwayo
tom boy. namnukuu chidi mimi ni msanii pekee nilifanya show nyingi
pengine kuliko wasanii wenzangu kwa hivyo nina uzoefu mzuri wa stage kwa
kuwa nimeshapanda hadi stage za magogo ya miti so siku ya uzinduzi wa
video ya tom boy ya bwana mdogo Baghdad nitawaonyesha fun wangu pakavu
nitakavyoteleza! Huku Baghdad akisema chidi ni msanii mzuri na nakiri
kusema laity kama aisngekuwepo chidi kwenye ramani ya mziki baasi
pengine Baghdad asingekuwa hapa alipofikia kwa sababu ukuaji wa mziki wa
Baghdad umetokana na chidi benz kwa kuwa ni rol modo wake ingawa
nisinukulike vibaya hata mwalimu wa jakaya kikwete ambae amemfanya kuwa
raisi pengine yeye hata ujumbe wa nyumba kumi hana. Sasa jibu
litapatikana ndani ya maisha club tar 17 mwezi wa 6 juma pili hii ambapo
kwa mara nyingine voice of the lady, kipenzi cha walimbwende, mwenye
p.h.d ya malovidovie hemedy nae kukutana na mzee wa baadae sana ikiwa ni
muda sasa umepita tangu waonane kwenye hatua za mwisho za kutengeneza
video yake aliyofanya na raper mwenye flow makengeza toka b hit mabeste
ambae anafanya vizuri na ngoma 2 zote akiwa na juzx baadae sana na
sirudi tena. Huku msanii toka mundi la zamamni alilokuwa ailitumikia
Baghdad mzee wa kunesanesa ndani, na show haitokwisha bila kumuona
nurdin anaetamba na rec yake ya kitolondo. Ni kwa kiingilio cha 7000
ndani ya maisha club. Usikose kuja kupata jibu la nani mkali wa stage,
na video mpya ya mjukuu wa lucifa.
No comments:
Post a Comment