Ndugu mdau wa Sanaa,
Wadau
wa Sanaa wanataalifiwa kuwa Gaba Art Centre wataendesha warsha ya masaa
mawili kuhusu Stadi za uandishi wa miswada ya Sinema ( Script writing
skills), Siku ya Jumatatu 18,June 2012, saa 4 kamili kwenye jukwaa la
sanaa katika ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)
Baadhi ya mambo yatakayojadiliwa ni;
1. Namna ya kuendeleza wazo hadi sinema ya kusisimua (Idea to a good film)
2. Namna ya kufikia hisia za watazamaji (Reaching Audience emotion)
3. Ujenzi wa Action na Dialogue nzuri.
3. Kutengeneza Wahusika (Characters)
4. Mfumo wa hadithi, Mwanzo, kati na Hitimisho ( Ploting, beginning, middle and end)
Ni
fursa nzuri kwa Wasanii kuleta mabadiliko kwenye tasnia ya filamu
kwani kumekuwa na changamoto mbalimbali katika tasnia hii ambazo kwa
njia moja au nyingine zimekuwa kikwazo katika kufikia ufanisi
unaohitajika
Mbali ya kukualika wewe binafsi, ninakuomba uwaalike wanachama wako wote wanaoweza kunufaika na mafunzo haya.
KARIBUNI SANA
No comments:
Post a Comment