M
|
ABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya
England, Manchester
City watafungua kampeni
ya kutetea taji lao kwa kuumana na klabu iliyopanda msimu huu ya Southampton.
Mahasimu
wa City, Manchester United wenyewe wataanza kampeni zao kwa kupimana ubavu na
Everton, katika ufunguzi huo unaotarajiwa kufanyika Agosti 18 mwaka huu.
Reading
iliyorejea Ligi Kuu, itakuwa na kazi ya ziada katika ufunguzi huyo itakapocheza
Stoke City, wakatika ambapo Wagonga Nyundo wa
London West Ham watatoana ngeu na Aston Villa.
Pambano
la mahasimu wa jiji la Manchester,
linalosubiriwa kwa hamu limepangwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Etihad jijini humo
hapo Desemba 8, kabla ya kurudiana kwenye Uwanja wa Old Trafford Aprili 6
mwakani.
Kocha
mpya wa Wekundu wa Anfield Liverpool, Brendan Rodgers ataanzia harakati za
kuirejeshea klabu hiyo heshima kwa kuwafuata West Brom,
inayonolewa na kocha wa zamani wa ‘Reds’, Steve Clarke.
Liverpool,
ambayo ilikuwa na msimu mbaya uliopita chini ya Kenny Dalglish, imejikuta
ikipangwa kuanzia nyumbani dhidi ya timu ngumu za Manchester City,
Arsenal na Manchester United, kabla ya kuzifuata ugenini mzunguko wa pili.
Washika
Bunduki wa London Arsenal, watanzia nyumbani kwa kuwaalika wageni wao
Sunderland na mechi ya kwanza kwa Roberto Di Matteo kama kocha rasmi wa Chelsea
ambao ni mabingwa wa Ulaya kwa kucheza na Wigan, huku Tottenham wakipangwa
kuanza na Newcastle.
London derby inayohusisha mahasimu wa jiji hilo
itaanzia kwa Chelsea
kuwafuata Arsenal hapo Septemba 29, kabla ya Gunners tena kuvaana na mahasimu
wao wengine Tottenham hapo Novemba 17 kwenye Uwanja wa Emirates.
Kwa
mujibu wa ratiba ya FA, Manchester City wataumana na Norwich
nyumbani katika hitimisho la msimu, huku majirani zao Man United wakiwafuata West Brom. Chelsea
itamaliza na Everton kwenye dimba la Stamford
Bridge, huku Arsenal ikitarajiwa
kumaliza na Newcastle.
No comments:
Post a Comment