• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Tuesday, September 4, 2012

    PRESS CLUB YATOA TAMKO MAUAJI YA MWANDISHI HABARI

    WAANDISHI na Wanachi mkoani Mbeya wamelaani vikali Mauaji ya Mwandishi wa habari wa Iringa Daudi Mwangosi,  aliyeuwawa Janai katika vurugu zilizotokea katika kijiji cha Nyororo mkoani humo.
    Marehemu Mwangosi ambaye alikuwa ni Mwenyekiti wa Klabu yawaandishi wa habari mkoa wa Iringa pia alikuwa akifanya kazi katika kituo cha Chanel Ten aliuawa wakati akiripoti vurugu zilizotokea kijijini hapo baina ya  Chadema na Polisi ambapo inasemekana alilipuliwa na bomu la machozi. Aidha kutokana na mauaji hayo waandishi na wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari  ya Mbeya chini ya Mwenyekiti wake Christopher Nyenyembe, kwa pamoja wamekubaliana kutoandika habari zozote zinazohusu jeshi la polisi kwa kipindi kisichojulikana. Pamoja na tamko hilo la kutojihusisha na kazi yoyote inayohusu jeshi hilo pia imeamriwa Jeshi hilo kutoa taarifa stahili juu ya hatua gani walizowachukulia wahusika wa mauaji hayo ambapo pia Viongozi waandamizi wametakiwa kujiuzulu haraka iwezekanavyo. Viongozi waandamizi waliotajwa kujuizulu ni pamoja na Mkuu wa Jeshi hilo IGP Mwema ,Kamanda wa polisi Mkoa wa Iringa na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi kwa kile kilichodaiwa kuendelea kufumbia macho mauaji ambayo yanaendelea kutokea katika maeneo mbalimbali ambayo yanahusisha jeshi hilo. Pia katika maoni yao wanahabari mkoani hapa wamevitaka kuundwa kwa tume huru ya kuchunguza mauaji hayo ambapo imependekezwa kutohusishwa kwa jeshi la polisi kutokana na kuhusishwa na mauaji hayo. Baadhi ya wajumbe waliotoa maoni yao katika Mkutano wa Dharura uliofanyika katika ofisi za Chama cha wandishi wa habari zilizopo katika mtaa wa Bhojani Katikati ya Jiji la Mbeya wamelaani kitendo hicho ambapo wamesema jeshi hilo limeshindwa kutambua kuwa mafanikio ya ulinzi shirikishi na polisi jamii yametokana na ushiriki mzuri wa wanahabari. Wamesema kuwa kutokana na Jeshi hilo kushindwa kutambua mchango wa waandishi wa habari katika kufanikisha shughuli zao ni  bora waandishi wote nchi nzima wakaungana ili kulaani vitendo vya jeshi hilo na mauaji ya Mwangoka. Hata hivyo baadhi ya wananchi wamewataka wanahabari kutokata tamaa  na kuzidi kusonga mbele bali wachukulie ni ushindi wa wanahabari na wananchi wote kufuatia kifo cha Mwangosi hivyo ili kumuenzi ni lazima kila mwanahabari akafanya kazi kwa bidii.

    No comments:

    3500K