• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Wednesday, November 28, 2012

    King Majuto amlilia Sharo Milionea



    King Majuto 

    Kwa ufupi
    “Nilimuongoza kwenye mambo mengi na siku zote nilikuwa nikimsihi asikimbilie kuoa kama walivyo vijana wengine ambao wakipata hela kidogo wanachokimbilia ni kuoa.
     Majuto alipatwa na hali hiyo baada ya kupata taarifa za msiba huo na hadi anazungumza na gazeti hili, ingawa alikuwa na nafuu, mwili wake ulikuwa umevimba.

    Akizungumza na Mwananchi Majuto alisema: “Kimeniuma sana kifo cha mwanangu Sharo.
    “Nimeshirikiana naye kwa mambo mengi, nilifahamiana naye tangu mwaka 2009 tulikutana pale Vijana Production, na tangu nimefahamiana naye, kuna mambo mengi sana tumefanya,” alisema Majuto ambaye mara baada ya kupata taarifa ya kifo cha msanii huyo alipata na shinikizo la damu.


    “Nilimuongoza kwenye mambo mengi na siku zote nilikuwa nikimsihi asikimbilie kuoa kama walivyo vijana wengine ambao wakipata hela kidogo wanachokimbilia ni kuoa.
    “Nilikuwa ninamwambia jenga maisha yako kwanza, hakikisha unakuwa na nyumba, gari na miradi, ili hata ukioa mtoto asipate shida nashukuru alinisikiliza alianza kupata mafanikio kifo ndo kimemchukua.

    “Sijui nisemeje kifo kina siri nzito, ningejua anakufa lini ningekata rufaa na hata kutoa rushwa lakini hiyo ni siri ya Mungu pekee...alikuwa ameanza kupata mafanikio masikini, sijui ni macho mabaya ya watu, sijui Mungu pekee ndio anajua kwa sababu alikopatia ajali wala hakukuwa na kona kali.

    “Alikuwa meneja wangu, matangazo yote mnayoyaona yeye ndio alikuwa akiingia mikataba yote na fedha zote, hakuwa mdhulumishi, kazi zote tulizofanya pamoja na yeye ndio alikuwa akisimamia, akiniambia mzee tusifanye hii kazi nami sifanyi.

    “Alikuwa ana msimamo wake, akisema Sh1milioni ni hiyo hiyo habadiliki tofauti na mimi na roho ya huruma, nikimtajia mtu bei akiniomba basi napunguza, sifanyi hivyo kwa njaa, hapana, ila ni ile imani niliyonayo sasa tofauti na Sharo.

    “Sidhani kama pengo lake kwangu litazibika na sijui kazi zangu nitazifanyaje tena bila yeye, alikuwa ni kila kitu kwangu pamoja na kumzidi umri.”
    Mwenyekiti Simba
    Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage alitoa pole kwa wadau wa filamu na kumuelezea marehemu Sharo Milionea kuwa hakuwa msanii wa kawaida kwani ni miongoni mwa kizazi kipya cha vijana wa Kitanzania walioamua kutafuta maisha kwa kutumia vipaji walivyopewa na Mungu.

    Yeye alijitumbukiza zaidi katika uchekeshaji na baadaye akaonyesha uwezo mkubwa katika fani ya muziki.
    Maisha ya Sharo Milionea
    Kila kona za miji na vitongoji vyake nchini, huwezi kukosa kusikia watoto wakisema ‘umebugi meen...nataka kula meen’ na yote hiyo ni staili na ubunifu wa msanii huyo.

    Sharo Milionea aliyejizolea umaarufu kwa staili yake ya utembeaji na uongeaji, na aliwateka mashabiki wa vichekesho hususani vijana na watoto kutokana na kubuni staili yake ya kuiga madoido ya watu wa Marekani, na kujiweka katika maisha ya juu ambayo kwa hakika hawezi kuyafikia.

    Ingawa aliigiza maisha hayo yeye binafsi hakupenda kabisa staili hiyo ya maisha na lengo la kuigiza ni kuwafundisha wenye tabia kama hizo kuacha, kwani binadamu wote ni sawa na hakuna aliyebora kuliko mwingine.

    Alizaliwa Septemba 12, 1987 Muheza, Tanga. Alijiunga na Shule ya Msingi Lusanga na baadaye akasoma Sekondari ya Kwabutu, Tanga.
    Alipomaliza shule mwaka 2005, alihamia jijini Dar es Salaam kumfuata mama yake aliyekuwa akiishi jijini kwa muda mrefu.
    chanzo mwananchi gazeti

    No comments:

    3500K