• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Monday, September 3, 2012

    Watanzania kupata simu za Blackberry kwa gharama nafuu.


    ·        Simu aina ya Blackberry Curve 8520 kuuzwa kwa shilingi 399,999 na Blackberry Curve 9300 kwa shilingi 599,999 tu.
    ·       Wateja watapata huduma za BIS na BBM bure na kifurushi cha kuanzia kwa siku thelathini.
    Dar es Salaam, 3rd September, 2012 … Watanzania walio wengi sasa watapata uwezo wa kununua simu za Blackberry Smart phone mpya zitakazo ingizwa sokoni kwa bei nafuu.
    Hii inafuatia, baada ya kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania, kupunguza gharama za vifurushi vya simu hizo za Blackberry mapema wiki iliyopita. Wateja wa Vodacom sasa watafurahia ofa mpya ya punguzo la simu hizo kupitia mpango  maalum wa kampuni hiyo wa  kurahisisha mawasiliano kwa wateja wake.
    Kampeni hii itahusisha mauzo ya simu aina ya Blackberry Curve 8520 itakayouzwa kwa shilingi 399,999 na Blackberry Curve 9300 ikiuzwa kwa shilingi 599,999. Kupitia ofa hiyo maalum. wateja wa mtandao wa Vodacom watakao nunua simu hizo watafurahia huduma mbalimbali za Blackberry kwa siku thelathini mfululizo.
    Akizungumzia mpango huo Mkurugenzi mkuu mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene Meza, amesema kuwa kupitia ofa hiyo wateja watafurahia huduma mbalimbali za Blackberry Absolute Plan (inayojulikana kama BIS) ikiwa pamoja na matumizi ya  BBM bure, Barua pepe za Blackberry, Blackberry AppWorld, Mitandao ya kijamii ya facebook na Twitter, foursquare, Linkedln na huduma nyingine za Whatsapp, Google Chat, akaunti kumi za barua pepe pamoja na Instant Messaging. BlackBerry Protect na BlackBerry Enterprise Server Express.
    “Ofa hii ya Blackberry itakuwa na manuufaa mengi kwa Watanzania, ninawasihi wateja wetu waweze kuzinunua na kufurahia huduma mbalimbali kutoka katika simu hizo,” alisema Meza na Kuongeza kuwa, “Kwa mpango huu nafuu kila mtu anayo sababu ya kununua simu hizi na kuendelea kufurahia ulimwengu mpya wa maendeleo ya sayansi na Teknolojia,”

    No comments:

    3500K