• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Wednesday, September 5, 2012

    DULLY SYKES ANATAFUTWA NA WANAJESHI

     Mkali mwenye hit kibao kila mwaka kila akitoa na sasa ana hit moja kubwa sana inayokwenda kwa jina la mtoto wa kariakoo prince dully sykes anatafutwa na majamaa yanayosemekana kuwa ni wanajeshi.  tukio ilo lilitokea juzi katika ukumbi wa mzalendo ambapo dully ilitokea kupishana lugha na mjeda mmoja aliekuwa kavaa kiraia na hapo ndipo mjeda yule akatishia kumtupa dully kutoka juu ya ghorofa hiyo ya mzalendo mpaka chini, hapo ndipo dully alipomruhusu bounsa wake kufanya kazi yake anaejulikana kwa jina la arafat ngumi jiwe. bunsa huyo kama kawaida yake na jina lake lilivyo akamtwanga sana jamaa huyo bila yakujua kama ni mjeda. akiongea na xdeejayz arafat ngumi jiwe amesema sisi tumeamua kujihami kwani yule jamaaa alikuwa anataka kumtupa dully kutoka ghorofani hivyo ndio tukajihami kwa kumpiga.  akaulizwa" unajuakama jamaa uliempiga ni mwanajeshi? akasema yeye ajui ni nani? chanzo chetu cha habari kinasema dully sykes ameamua kujificha kutokana na salam amnazozipata kama kuna wanajeshi wanakutafuta leo siku ya pili.
    Dully sykes akiwa na baunsa wake Arafat ngumi jiwe

    No comments:

    3500K