• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Wednesday, August 1, 2012

    GLOBAL POLITICAL NEWS: WAASI NCHINI SYRIA WAPATA MIZINGA YA ANGANI


    Waasi wanaopigana kuuondoa madarakani utawala wa Rais Bashar al Assad wa Syria kwa mara ya kwanza wamepata silaha za mizinga ya kurushwa kutokea angani. 
    Kituo cha televisheni cha NBS kimeripoti kuwa Jeshi Huru la Waasi wa Syria, FSA, limepata kiasi kidogo cha silaha hizo ambazo ziliwafikia kupitia jirani yao Uturuki ambayo imekuwa ikimtaka Rais Assad aachie ngazi kufuatia wimbi la mauwaji. Maafisa wa Marekani walisema hapo awali kuwa nchi jirani na Syria zinazotaka utawala wa Assad uondoke ikiwemo Saudi Arabia na Qatar zinashinikiza waasi wapewe silaha za aina hiyo. Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mashambulizi ya angani kutoka kwa vikosi vya serikali hasa kwenye mji wa Aleppo, na kuwafanya waasi kuhitaji silaha hizo kwa dharura. 
    Hata hivyo NBS haikutaja ni aina gani ya silaha hizo zijulikanazo kama MANPADs wamepewa waasi hao. Kwa kawaida zipo za teknolojia ya chini hadi za hali ya juu.

    No comments:

    3500K