• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Friday, August 31, 2012

    AFRICA POLITICAL NEWS: WAISLAMU MOMBASA KUANDAMANA LEO BAADA YA SALA YA IJUMAA

    Habari kutoka miji ya Nairobi na Mombasa nchini Kenya zinasema kuwa, Waislamu wanapanga maandamano makubwa katika miji hiyo punde baada ya Sala ya Ijumaa hii leo  kulalamikia mauaji ya viongozi na wanaharakati wa Kiislamu.
    Duru za polisi jijini Nairobi zinasema kwamba, maafisa wa kuzima fujo wamewekwa katika hali ya tahadhari iwapo maandamano hayo yatageuka na kuwa fujo. Mkuu wa polisi jijini Nairobi amesema hakuna kibali kilichotolewa kwa ajili ya maandamano hayo lakini Waislamu wamesisitiza kuwa wataandamana. Mwanaharakati wa Kiislamu, Sheikh Aboud Rogo aliuawa siku ya Jumatatu mjini Mombasa na watu wasiojulikana. Mauaji hayo yalizusha machafuko na fujo baada ya vijana wenye hasira kuandamana na kuchoma moto makanisa mjini humo. Maafisa wanne wa polisi tayari wameuawa kwenye fujo hizo za Mombasa

    No comments:

    3500K