• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Saturday, June 9, 2012

    JESHI LA POLISI MKOANI KIGOMA WAOKOA WATU WATATU WANAOTUHUMIWA KUWA WACHAWI:

     BAADHI YA WANANCHI WAKISHANGAA BAADA YA FAINES KUZINDULIWA NA MTOTO MWENYE MIAKA KUMI ALIYEKABIDHIWA MIKOBA NA MAMA YAKE.
     BIBI NA MJUKUU WAKE WANAOSADIKIWA NI WACHAWI WAKIWA KATIKA GARI LA POLISI.
     FAINES AKIPAKIWA KATIKA GARI YA POLISI.
    FAINES ZAWADI-BINTI ALIYEFARIKI KWA MUDA NA KUREJESHWA DUNIANI AKIWA AMESHIKILIWA NA NDUGU ZAKE.
     
    Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limefanikiwa kuwaokoa watu watatu waliokuwa wamezingirwa na kundi la wananchi wakitaka kuwaua kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ushirikina.
    Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma SSP Joseph Konyo, aliwataja watu hao waliokolewa kuwa ni Evania Sephanga(50), mkazi wa wilaya ya Kibondo, Bruno January(46), mkazi wa kijiji cha Nyamhoza na mtoto mmoja mwenye umri wa miaka kumi na mkazi wa kijiji cha Nyamhoza Kigoma mjini ambaye jina lake linahifadhiwa.
     
     
    Kamanda Konyo amesema kuwa wiki iliyopita majira ya saa tisa mchana, watu hao walizingirwa na kundi hilo kwa madai kuwa walimroga na kumuua msichana mmoja aitwaye Faines Zawadi(20) mkazi wa kijiji hicho cha Nyamhoza ambaye siku moja kabla ya kifo chake alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa na kuwa kama kichaa.
    Alisema katika tukio hilo, bibi kizee mmoja ambaye alikuwa mshirika wa kundi la waliodaiwa kuwa wachawi, alifanikiwa kutoroka katika mazingira ya kutatanisha alipojifanya kuwa anakwenda kujisaidia.
     
     
    Kamanda Konyo amemtaja bibi huyo aliyefanikiwa kutoroka kuwa ni Bibi Editha Dosiyo mkazi wa kijiji hicho ambaye baadaye alipatikana na kuhojiwa kabla ya kukabidhiwa kwa Idara ya ustawi wa jamii baada ya kuonekana kuwa maisha yake yangekuwa hatarini.
    Amesema baada ya Polisi kupata taarifa za tukio hilo, walikimbia na kwenda kuwaokoa kutoka katika mikono ya kundi la wananchi lakini wakiwa wameshaadhibu ingawa ilikuwa haijawa kwa kiasi kikubwa.
    Habari zinasema kuwa, baadhi ya wananchi walipata taarifa kutoka kwa mtoto aliyeokolewa akisema kuwa baadhi ya watoto waliofariki kijijini hapo, akiwataja (majina tunayahifadhi) alikuwa akiwaona nyumbani kwao nyakati za usiku wakiosha vyombo na baadaye kupewa chakula.
    Siku ya tukio hilo, baadhi ya wananchi walisema kuwa kabla ya bibi huyo kutoweka alimnong’oneza jambo mjukuu wake ili amfanyie mareheme ikiwa ni pamoja na kumruka mara saba kisha bibi huyo alitoweka akijifanya anakwenda kujisaidia.
     
     
    Walisema mara baada ya bibi huyo kutoweka, mtoto huyo wa kiume ambaye ni miongoni mwa waliozingirwa wakitaka kuuawa, aliamza kutekeleza maagizo ya bibi huyo na alipomaliza kitendo cha kumruka kwa mara ya saba, msichana yuyo ambaye alikuwa ni marehemu alizinduka na kuomba uji.
    Wamesema msichana huyo ambaye alikuwa mfu, alipewa uji na kunywa kisha akapelekwa hospitalini ambako hadi sasa hali yake inasemekana kuwa inaendelea vizuri.
    Hata hivyo Kamanda Konyo ametoa wito kwa wananchi kuacha kuchukua sheria mkononi na badala yake watoe taarifa Polisi kwa kila jambo wanaloliona kuwa linaweza kuleta uvunjifu wa amani ili hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya wahusika.
    Mwezi uliopita watu wawili mke na mume, waliuawa na kundi la watu wenye hasira kisha miili yao kuchomwa kwa moto mkoani Kigoma baada wa kutuhumiwa kuwa walikuwa ni wachawi.

    No comments:

    3500K