• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Thursday, June 21, 2012

    Aota matiti baada ya kutumia ARV`S


    Mkaazi wa kijiji cha Magomeni Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani,
     Khamisi Tanga (46), ameota  matiti katika hali isiyo ya kawaida
    ikidaiwa imesababishwa na kutumia dawa za kupunguza  makali ya Ukimwi 
    ARV’S.
      Akizungumza na waandishi wa habari waliokwenda Wilayani humo
    kufanya utafiti kuhusu utekelezaji wa sheria ya Ukimwi na Chama cha
    Waandishi wa habari za Ukimwi (AJAT),Khamisi (Pichani) alisema alipatwa
    na mkasa huo miaka mitatu iliyopita.
     Akisimulia namna alivyoanza kuugua alisema awali aliona matiti
    yake yakiongezeka ukubwa kila kukicha lakini hakujua kama lingeweza kuja
    kuwa tatizo kubwa kama lilivyo sasa.
     Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya ilimbidi kwenda kliniki
    anayohudhuriaga kupata dawa na kuwaeleza manesi ambapo walimjibu kuwa
    imesababishwa na dawa anazotumia na hivyo kulazimika kukatizwa dozi hiyo
    na kupewa aina nyingine.
     Hata hivyo Khamisi alisema kwamba pamoja na kubadilishiwa dozi
    hajaona kama kuna mabadiliko yoyote aliyoyapata na kuongeza kwamba hivi
    karibuni alipewa dawa nyingine ambazo kati ya hizo kuna zile ambazo
    zilimsabishia matiti na tayari ameanza kupatwa na maumivu aliyokuwa
    akisikiaga awali wakati matiti yalivyokuwa yanaanza kuota.
      Kwa mujibu wa Khamisi ameshahangaika kupata matibabu hadi
    Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili lakini hadi leo hajapatiwa tiba stahili
    ya kumaliza tatizo hilo.
    “Jamani Watanzania naomba wanisaidie kwa njia yoyote ile ili
    niondekane na hali hii kwani inanidhoofisha sana na kunikosesha raha
    hasa mbele ya wanaume wenzangu."Kwani hapa navyoongea na nyie waandishi nilipimwa hadi kansa na matiti ndio kama hivyo mnavyoyaona yanaendelea kukua na huniuma sana
    hasa wakati ninapolala,”alisema kaka huyo.Pia alitumia fursa hiyo kumuomba Rais Jakaya Kikwete kumsaidia ili
    arudi katika hali yake ya uanaume kwa kuwa maisha kwa sasa kwake
    yamezidi kuwa magumu kwa kuwa hawezi kufanya kazi yoyote kutokana na
    hali hiyo.
    Mtaalam wa magonjwa, Dk. Dina Komakoma,akielezea kuhusu sababu za
    kutokewa kwa hali hiyo kwa wagonjwa wenye maambukizi ya VVU ni jambo la
    kawaida japo hutofautiana.
    Dk. Komakoma alisema wengine hujikuta wakinenepa au wakikonda sana na
    hili la Khamis sio mtu wa kwanza kupatwa na hali hiyo na kuongeza kwamba
    inapotokea mgonjwa akapata hali tofauti kama hiyo anapaswa kusitishiwa

    No comments:

    3500K