• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Monday, October 15, 2012

    Tanzania Nayo Kuzima Simu Zote za Kichina Kama Kenya


    Tanzania inatarajia kuchukua hatua kama iliyochukuliwa nchini Kenya ya kuzichinjia baharini simu zote za bandia ambazo nyingi ni za kichina kwa kuzizima kabisa.

    Taarifa hiyo imetolewa na kaimu meneja mawasiliano wa mamlaka ya mawasiliano (TCRA) Semu Mwakyanjala ambaye amesema mamlaka hiyo itaanza kwa kutoa elimu kwa umma kuhusiana na umuhimu wa kununua simu halali.


    Ameliambia gazeti la Daily News Jumapili kuwa hatua hiyo itachukuliwa na nchi zote wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki zikiwemo Rwanda, Uganda na Burundi.

    Kuna taarifa kuwa makampuni mengi ya simu nchini Tanzania yameupokea mpango huo kwa shingo upande kwa hofu kuwa yatapoteza wateja wengi.

    Kwa upande wa tume ya mawasiliano ya Uganda (UCC) hatua hiyo ya kuzima simu bandia itafanyika mwishoni mwa mwezi November

    No comments:

    3500K