• Breaking News

    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    It's more about music industry and social issues in and out of bongo land

    Monday, October 1, 2012

    Suma Mnazaleti Asema Alikula Kiapo Kumtaja Star Aliemwimba kwenye wimbo wake wa Chukua Time...


    AKATI ngoma yake ya ‘Chukua Time’ ikiendelea kushika chati za juu, msanii Suma Mnazaleti, amesema kuwa watu wengi wamekuwa na hamu ya kutaka kumjua ni msanii wa bongo movie anayemzungumzia katika ngoma hiyo, lakini anashindwa kumtaja kwani tangu alipokuwa anaandika wimbo huo alikula kiapo kuwa hatokuja kumtaja jina kamwe.

    Mnazaleti alizungumza na DarTalk kuhusu jina la staa wa bongo movie ambaye anamzungumzia ndani ya ngoma hiyo, ndipo alipofunguka kuwa hawezi kumtaja mtu yeyote kwani ameshakula kiapo tangu alipokuwa anauandika wimbo huo.

    Alidai kuwa watu wengi watu wana majibu yao lakini kwa upande wake hawezi kuzungumza chochote kwani anaamini hataki kumdhalilisha staa huyo kwa tabia zake za kumsubua kwenye simu wakati awali alikuwa anamuona kama kuku mchafu.

    “Watu wengi wamekuwa na majibu yao kuwa ninayemuimba ni kati mtu fulani au fulani lakini kwa upande wangu ni nimekula kiapo cha kutomtaja niliyemzungumzia hivyo nawaomba mashabiki wangu wajue kwamba hata kwa mtutu siwezi kumtaja jina atabaki kuwa siri yangu” alisema

    No comments:

    3500K