Pages - Menu

Thursday, January 24, 2013

MBUNGE WA ARUSHA AFUNGA SHULE


na jaizmelaleo

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema, ameifunga Shule ya Sekondari Korona iliyopo Kata ya Engutoto jijini hapa, ambayo ilizinduliwa na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, mwaka 2011.
Lema alifikia uamuzi huo katika kikao cha pamoja cha mashauriano shuleni hapo na Kaimu Mkuu wa Shule hiyo, Eusebi Maeda, kilichohudhuriwa pia na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji ambaye ni Ofisa Utumishi, Eliphas Mollel na Ofisa Elimu Sekondari, Violet Muwowoza.
Alisema kuwa aliifunga shule hiyo kutokana na kukabiliwa na matatizo mengi yaliyosababisha wanafunzi kushindwa kusoma tangu ifunguliwe Januari 14, mwaka huu.
Matatizo hayo ni pamoja na umbali unaosababisha wanafunzi na walimu kutembea kilometa 6.5 hadi kufika shuleni hapo, hivyo kuwa na muda mfupi wa masomo.
Shule hiyo pia haina huduma ya maji safi baada ya bomba lililokuwepo kukatwa na mamlaka ya maji kutokana na deni la sh 340,000. Pia, pamoja na walimu watano waliopo, mkuu wa shule na msaidizi wake hawaonekani.
Kati ya wanafunzi 1,200 wa kidato cha kwanza hadi cha tatu wa shule hiyo ni wanafunzi 118 pekee ndio wanaohudhuria masomo.

No comments:

Post a Comment