Pages - Menu

Monday, August 27, 2012

Safari ya Prezzo nchini Nigeria imemrudisha bila kukipata kile alichokiendea


Prezzo and Goldie
Safari ya Prezzo nchini Nigeria imemrudisha bila kukipata kile alichokiendea baada ya Goldie kuonekana kutofurahishwa na ziara yake. Prezzo aliyekuwa mshindi wa pili kwenye Big Brother Africa StarGame wiki hii alienda nchini Nigeria kuwaomba radhi wananchi wa huko na pia kutangaza nia ya kumfanya Goldie awe mke wake. Katika mahojiano na waandishi wa habari jijini Lagos, Prezzo alisema alienda nchini humo kumuomba uchumba Goldie. Hata hivyo hakufanikiwa kuonana Goldie ambaye Prezzo alisema hakuwa anapokea simu yake.

No comments:

Post a Comment